Zari: Kamwe Siwezi Kumuanika Mwanaume Wangu Mtandaoni
Mzazi mwenzake na staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan ‘Zari’ amefunguka na kuweka wazi kuwa kamwe hatakuja kumuanika tena Mpenzi wake kwenye mtandao.
Baada ya kuachana na Diamond mwaka mmoja uliopita Zari hajawahi kumuweka wazi mwanaume ambaye yupo naye kwenye mahusiano ingawa ameshawahi kusema yupo kwenye mahusiano.

Zari alifikia hatua ya kuweka wazi hayo alipoulizwa kama kweli hana mpango wa kuolewa na Diamond na atamuanika lini mwanaume anayempenda ambapo alieleza kuwa mwanaume wake si wa mitandao ya kijamii.
Mume wangu siyo wa social media, ni mume wangu siyo wetu“.
Zari ambaye ana watoto watano wawili kati yao amezaa na Diamond baada ya kuachana na Mbongo Fleva huyo amewahi kuhusishwa kimapenzi na mwanaume anayeitwa Brian wa nchini Uganda ambapo mara mbili tofauti alionekana kupiga naye picha za ukaribu lakini mwenyewe alidai kuwa ukaribu wao huo ni wa kikazi tu.