Zari Awajibu Wanaomtaka Ahame Kwenye Nyumba Ya Diamond
Mfanyabiashara maarufu kutoka Uganda Zari The Bosslady ambaye pia ni mzazi mwenzake na staa was Bongo fleva Diamond Platnumz, ameibuka na kuwajibu mashabiki ambao wamekuwa wakimtaka ahame Kwenye Nyumba ya Diamond.
Miaka michache iliyopita wakati Diamond na Zari wapo kwenye mahusiano Diamond alinunua Nyumba ya thamani nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya Zari na Watoto Wake lakini Baada ya kuachana Zari bado anaishi kwenye nyumba ile.
Mashabiki mbali mbali kwenye mitandao ya kijamii wamekuwa wamtaka Zari ahame Kwenye Nyumba ya Diamond kwa sababu wamekwisha achana na yeye anajitamba kuwa ni tajiri.
Baada ya kuchoshwa na maneno hayo Zari amewajia juu amshabiki hao kupitia ukurasa wake wa Instagram na kusema kuwa hawezi kutoka Kwenye Nyumba hiyo kwani yeye na watoto wake walinunuliwa ili waishi.
Zari amewatolea watu wajue kuwa yeye kuishi pale sio kwamba hana Nyumba Bali ana Nyumba nne South Afrika lakini anaishi pale kwa sababu ni Nyumba yake aliyonunuliwa na baba wa Watoto wake.