Young Killer Adai Wasafi Festival ni Ukombozi Wa Kweli Kwenye Burudani
Msanii wa muziki wa hip hop nchini Young Killer ameibuka na kulimwagia sifa kibao Tour ya WCB ya Wasafi Festival Baada ya kushiriki katika tamasha Lao la kwanza mkoani Mtwara.
Young Killer Msodoki amefunguka kwa kulisifu tamasha la Wasafi Festival na kudai kuwa ni ukombozi halisi katika sekta ya Burudani Nchini Tanzania.
Katika mahojiano aliyofanya na Bongo 5, Young killer amefunguka haya zaidi kuhusu shoo hiyo:
Ujio wa Wasafi Festival ni mkubwa na umekuja kiutofauti sana na kiukweli tasnia yetu inahitaji vitu kama hivi kwa sababu haya ni mapinduzi kwani muda mrefu tumekuwa tukimiss matamasha yamekuwa machache kwaiyo kuja kwa Wasafi Festival ni jambo la kumshukuru Mwenyezi Mungu kwani inaonyesha ni kwa jinsi gani Sanaa yetu hivyo Big Up sana kwa Wasafi”.
Young Killer pia atakuwa mmoja wa wasanii Watakaoperfom kwenye shoo nyingine ya Wasafi Festival itakayofanyika Mkoani Iringa siku ya Leo.