Watu Wanafanya Dhambi Makusudi na Kumsingizia Shetani-Martha
Mwanadada Martha Mwaipaja ambae wiki hii alipata nafasi ya kuonekana katika kipindi cha kikaangoni live cha EATV, amefunguka na kusema mengi huku akiwashangaa sana watu ambao wamekuwa wakifanya makosa ambayo wanajua kabisa kuwa ni dhambi lakii wanafanya kwa makusudi .
Martha anasema kuwa watu wamekuwa wakimsingizia shetani kwa amewapitia alkaini uapokuja kuona jinsi dhambi hiyo ilivyotendeka unaona kabisa kuwa watu hao walikuwa wamepanga kufanya kitu hicho.
Kwa kutolea mfano, martha anasema kuwa kuna dhambi kama ya kuzini ambayo imekuwa ikitendwa karibia kila kukicha lakini hata ukiangalia mazingira watu yanayofanyia kityu hicho unaona kabisa kuwa ilikuwa imekusudia huku akisema kuwa kwa nini kama ni shetani amewapitia basi wanaacha kufanya kitendo hicho sebleni na kupelekana chumbani.
Martha amefunguka na kuwashauri watu kubadilika na kmrudia mungu kwa kuamua kutenda matendo yaliyo mema na ya kumpendeza yeye.