“Wasanii Kuweni na Misimamo na Hata Mnapotakiwa Tajeni Dau Manalolitaka”-Diamond Platnumz
Msanii wa muziki wa Bongo fleva na CEO wa WCB Diamond Platnumz ameibuka na kuwataka wasanii kuwa na msimamo na kuchagua malipo yanayoweza kuwafaidisha wao na familia zao.
Maneno hayo yamekuja ikiwa ni muendelezo wa mivutano kati ya Wasafi na Clouds Fm ambapo Diamond na timu yake nzima wamekuwa wakimtuhumu Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Clouds kwa kuwanyonya na kuwaonea wasanii.
Baada ya mvutano wa muda mrefu na majibizano yao ya siku mbili hizi kuchochewa na shoo zao zitakazofanyika jumamosi ambapo Fiesta mwaka huu imeweka wasanii wengi ambao ni wakongwe na Wasafi wanaamini wamefanya hivyo Baada ya kuwapa changamoto.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Diamond amewndelea kuwatupia vijembe Clouds na kuandika haya: