Tanasha Azidi Kujiamini na Penzi la Diamond
Mpenzi wa staa wa Bongo fleva na Mkurugenzi wa WCB Diamond Platnumz, Tanasha Donna Oketh ameonekana kuweka maneno ya watu pembeni za kuzidi kukolea Kwenye Penzi na Diamond.
Tangu Diamond aweke hadharani kuwa yupo kwenye mahusiano na Tanasha mwaka jana mwishoni ni wazi kuwa hawajapita njia nyepesi kwani Penzi Lao linapingwa sana hasa kwenye Mitandao ya kijamii.
Lakini Diamond na Tanasha wameonekana kupuuzia maneno ya watu na kufanya mambo yao na inaonekana wazi kuwa Tanasha amekolea kwenye Penzi na Mbongo fleva huyo.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Tanasha ujumbe ambao ni mfupi Lakini unabeba maneno mazito kuhusiana Penzi lake na Diamond:
Kujiamini ya kweli huwa haina chumba cha chuki, ni pindi unapofahamu kitu kizuri hauna sababu ya kuchukia”.