Aslay: Sivuti bangi

Aslay amefunguka kuhusu mtindo wake wa maisha na jinsi anavyo nawiri kama solo artist. Msanii huyo alieza kuwa bado yuko Yamoto Band hata kama anatoa nyimbo zake pekee yake.

Watu wengi wanadhani Aslay ametoka Yamoto Band lakini ukweni ni kwamba hakuna msanii yeyote ambaye amekihama kundi hilo.

Yamoto Band

 

Akiongea na Times FM 100.5, Aslay alisema kuwa Mkubwa Fella amewakubali kila msanii wa Yamoto Band kufanya kazi kivyake. Aslay mwenyewe ashaachia nyimbo tatu kama solo artiste.

Aslay pia aliuliza maswali kuhusu mtindo wa maisha yake, mtangazaji wa Times FM alimuuliza kama huwa anavuta bangi.

“Hapana sivuti bangi, sinywi pombe” Aslay alimjibu.

Tazama mahojiano hayo kwenye video hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=xBaR9hiu3lk

Yamoto Band yatoa wimbo mpya baada ya kuzuka minong’ono mitaani juu ya ukimya wao

Ukimya wa Yamoto Band ulichangia kuzuka kwa uvumi kuwa kundi hilo limesambaratika. Kiongozi wa Mkubwa na Wanawe Said Fella alisisitiza kuwa bado Yamoto Band wako pamoja ingawa kila mmoja anaishi kivyake.

“Maneno yalikuwa mengi juu ya Yamoto Band yetu lakini sisi tulikuwa kimya na mengi yalisemwa na leo tumeleta wimbo mpya unaitwa Basi,” Mkubwa Fella aliambia Clouds FM.

Ukweli wa matamshi yake ulidhihirika pale ambapo Diamond alitangaza kuwa Yamoto Band wametoa wimbo mpya.

“Brand New Hit from @Yamoto_Band #BASI it’s now Exclusively Available on @wasafidotcom (Moja ya ngoma nilokuwa nikiisubiria kwa hamu toka yamoto band sasa imetoka inaitwa #BASI na inapatikana ndani ya @wasafidotcom Wadau tuwatie Moyo vijana wetu kwa kuinunua kwa mia 300 tu….Maana, Huu ndio Muda wa kumuunga mkono Msanii Umpendae…” Diamond aliandika kwa Instagram.