Ujumbe wa Diamond kwa Mzee Yusuph kufuatia kifo cha mkewe na mtoto wake

Mzee Yusuph alimpoteza mke wake mdogo Chiku Khamis Tumbo na mwanawe mchanga ambao waliaga dunia usiku wa Jumamosi katika hospitali la Amani Dar es Salaam Tanzania.

Chiku alifariki akijifungua, mtoto wake wa kike pia aliaga dunia wakati huo. Mwenda zake alikimbizwa hospitalini na Mzee Yusuph usiku huo alipoanza kuskia uchungu wa kujifungua.

Mashabiki wa Mzee Yusuph wamekua wakitoa salamu za rambirambi kwenye mitendao za kijamii kufuatia kifo cha bibi yake.

Chiku Khamis Tumbo

Diamond Platnumz pia amemfariji Mzee Yusuph kwa ujumbe aliyoandika kwa Instagram; alimpa roho kwa kumwambia Mola ndo hupanga kila kitu duniani.

“Stay strong bro, Mwenyez Mungu ndio mpanga wa kila jambo… tumshukuru na kuwaombea waendapo wapumzike kwa Amani…Amin, Inshaallah?” Diamond aliandika.

 

Huu ndo ujumbe Rapper Jay Moe alitoa baada ya kusemekana kuwa ako na ubishi na Diamond Platnumz

Mahojiano aliyofanya Jay Moe katika The Playlist ya Times FM umezua utata, blog ya Udaka TZ ulimnukuu Jay Moe akisema kuwa hawezi kujiunga na WCB ata kama lebo hio wanamuitaji.

Blog hio pia lilisema kuwa rapper huyo hawezi peleka ngoma zake kwenye platform ya Wasafi.com ya kuuza muziki kwenye mtendao.

Hata hivyo Jay Moe amejitokeza na kupinga madai ya Udaku TZ, rapper huyo amesema hana ubishi wowote na Diamond.

“@udakutz_ Naheshimu Sana Kazi Za Mikono Yetu,Sijawahi Kufanya Interview Na Nyie Wala Kunicontact For An Interview…Tafadhali Naomba Muache Kucopy Na Kupaste Vitu Namna Hii,I have Huge Respect For @diamondplatnumz Na #WASAFI Kwa Ujumla,Tufanye Vitu Vya Kujenga Sio Kubomoa…Sina Tatizo Na Kupeleka Nyimbo Zangu #wasafidotcom Na Hakuna Sehemu Nimesema Sitopeleka So Dont Get Twisted,Kusema Sitosign Its Because I Have My Own Label #SoFamous So Please Next Time Kama Mnahitaji Udaku Kama Huu Msisite Kinitafuta Lakini Sio Kufabricate Story @udakutz_ Kwa Niaba Ya #SoFamous Napenda Kusema Kwamba Hii Ni Wrong Info.. #Nisaidie_Kushare???” Jay Moe aliandika kwa Instagram.

Jay Moe

 

“Napatana na Zari aliyeniletea watoto hao wengine siwajui” Mamake Diamond amkana Hamisa Mobeto

Kulingana na umbeya mitaani, Diamond Platnumz amempa mimba Hamisa Mobeto – mrembo yule aliyekuwa kwa video ya ‘Salome’.

Mbeya Soudy Brown alimpigia simu mamake Diamond Sanura ‘Sandra’ Kasim kudhibitisha kama ni ukweli kuwa Hamisa Mobeto amebeba mtoto wa Diamond tumboni.

Hamisa Mobeto na Diamond

La kushangaza ni kuwa Sandra alimkana Hamisa Mobeto licha ya mrembo huyo kuonesha ukaribu zaidi na familia ya Diamond. Hamisa aliwai zua utata alipoonekana na mamake Diamond kwa picha.

Mamake Diamond aliambia Soudy Brown kuwa yeye anapatana tu na Zari ambaye amemletea wajukuu wala hana lolote na warembo wengi wote wanaohusishwa na Diamond.

Skila mahojiano kati ya Soudy Brown na mamake Diamond hapo chini:

https://www.youtube.com/watch?v=jnG2h6EG32E

Diamond: Watu hawajui mimi na Wema Sepetu tunaongea sana lakini sio kwenye media

Diamond and Wema Sepetu walikua wapenzi kabla ya hit maker huyo kumtema Wema na kumoa Zari Hassan, hatua ambayo ilizua utata sana.

Watu wengi waliamini kuwa Diamond alitaka mtoto ndo maana alimwacha Wema Sepetu ambaye mbaka wa leo hajajaliwa kupata mtoto.

Hata kama Diamond alimwacha Wema, wawili hao bado huwa wanaongea na kukutana bila ya vyombo vya habari kupata uhondo wowote.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, Diamond alidhibitisha kuwa bado ako na uhusiano mwema na Wema Sepetu ingawa wao hufanya vitu vyao jini ya maji.

Hit maker huyo wa ‘Marry You’ alifunguka na kusema kuwa yale maneno ya kuvutia kwenye manukato yake – ‘The scent you deserve’ ni Wema Sepetu ndo alitoa.

Chibu Perfume

“Mimi na Wema labda watu hawajui sisi tunaongea sana wakati mwingine tunakutana tu sana lakini sio kwenye media. Tushakuwa kila mtu ana mahusiano yake tofauti yeye ana familia yake hata ukiangalia katika Perfume yangu lile neno THE SCENT YOU DESERVE alilitoa Wema” alisema Diamond.

 

Dully Sykes aeleza kwanini anaegemea upande wa Diamond badala ya Ali Kiba

Dully Sykes ameshawahi kushirikiana na Ali Kiba na Diamond kuachia nyimbo; ‘Kuteseka Nimechoka’ (na Ali Kiba) na ‘Utamu’ (na Dianond na Ommy Dimpoz).

Sykes pia amejaribu mara nyingi kuwapatanisha Diamond na Ali Kiba lakini kila mara alipojaribu juhudi zake ziliambulia patupu.

Dully Sykes na Diamond

Akiongea kwenye kipindi cha 180 Power cha Sibuka FM, Dully Sykes alifunguka na kusema kuwa anaegemea upande ya Diamond kuliko upande wa Ali Kiba.

Mwimbaji huyo alieleza kuwa upande wa Ali Kiba hawataki kuwa karibu lakini upande wa Diamond wanamuonyesha upendo

“Upande wa Alikiba hawataki kuwa karibu na mimi ila upande wa Diamond wapo karibu na mimi, sababu hao wapo karibu na mimi na wao wananionyesha upendo ndio maana nipo karibu nao na sina tatizo na Ali Kiba wala Diamond,” alisema Dully Sykes.

 

Diamond aorodheshwa miongoni mwa wasanii wanaoamini ushirikina

Orodha ya wasanii wanaoamini ushirikina umetolewa, Diamond Platnumz yuko miongoni mwa wasanii waliotajwa kwenye orodha hio.

Meneja Maneno – aliyekuwa meneja wa Diamond, Rich Mavoko, Nay wa Mitego na wasanii wengine, amefunguka kuhusu wasanii anaodai wanaamini ushirikina.

Meneja Maneno anadai kuwa Diamond ndo gwiji wa ushirikina, alikiri kuwa kuna wasanii wengine ambao yeye mwenyewe aliwapeleka kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kuroga.

Meneja Maneno

Akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo cha EA Radio, Maneno aliwataja pia Rich Mavoko, Sam wa Ukweli miongoni mwa wasanii wanaoamini ushirikina.

“Ndele ni sehemu ambayo baadhi ya wasanii waliiamini sana lakini Mungu akisema ‘Yes’ ni ‘Yes’ tu kwa hiyo nakumbuka wasanii ambao nilikwenda nao kwa waganga kuroga ni pamoja na Rich Mavoko tena tulienda mbali kabisa huko Kigamboni ndani ndani huko tumeenda ndugu yangu, nilisharusha nazi katikati yaani usiku ule unajifanya chizi kama umevurugwa.

“Hata Sam wa Ukweli siwezi kukataa, ni watu ambao imani yao iliwapeleka huko lakini mimi nakumbuka kazi yangu niliyokuwa nafanya sikutaka kwenda kwa waganga…. ila sasa huyu Mondi sasa nimepata taabu naye, mara leo twende kwa mjomba, tunapeleka unga, leo tunapeleka mchele na mganga alivyo mshenzi hajawahi kuagiza samaki, yeye ni jogoo, mbuzi,” Meneja Maneno alisema.

 

 

Diamond: Wasafi hairuhusu wasanii wake kuandikiwa nyimbo

Wasanii wengi maarufu duniani huandikiwa nyimbo zao, kwa mfano Ne-Yo ingawaje ni mwimbaji ambaye ametajika, anajulikana pia kuandikia wasanii wenzake nyimbo.

Ne-Yo aliandika ‘Take a Bow’ iliyoimbwa na Rihanna, ‘Spotlight’ ya Jennifer Hudson, ‘Irreplaceable’ ya Beyonce, ‘Knock You Down’ ya Keri Hilson na nyimbo zingine kadhaa.

Hata kama imedhibitishwa kuwa wasanii wanaweza fanikiwa kimuziki bila kuandika nyimbo zao, Diamond hataki msanii kujiunga na lebo yake kama hajui kuandika nyimbo.

Akiongea kwenye kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Diamond alisema wasanii kutoka Wasafi huandika nyimbo zao wenyewe. Aliongezea kusema kwamba kabla ya kurecord wimbo wowote, wasani wote wa Wasafi hukagua wimbo aliyoandika msanii ili kubaini kama kuna makosa na kuelekezana.

“Kwanza Rich Mavoko ndiye mgumu kwenye kupitisha nyimbo, ikitoka hapo Ravvanny aipitishe, Queen Darleen aipitishe, ikitoka hapo niipitishe mimi, iende kwa Mkubwa Fella na Babu Tale waipitishe na Sallam aipitishe, ukitoka hapo wewe ni mwanaume haswa. Kwa hiyo wengi wanakuwa na uwezo mkubwa. Labda unaweza ukaja ukasikia kitu kidogo, ukasema ukiweka hapa kitu flani itakuwa poa zaidi, yaani ukiandika unaandika haswa,” ameeleza Diamond.

 

Kwanini Diamond ameshindwa kupost chochote kumtakia hali aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Zari

Mume wa Zari Hassan wa kitambo – Ivan Ssemwanga amelazwa hospitalini nchini Afrika Kusini. Ivan alikibizwa hospitalini baada ya kuugua ugonjwa wa Kiharusi (kwa Kiingereza stroke).

Siku chache zilizopita Zari aliwaomba mashabiki wake wamuombe mpenzi wake wa kitambo ambaye ni baba wa watoto wake watatu.

Soma pia: Zari awaomba mashabiki wake wamuombee mume wake wa kitambo – Ivan baada ya kulazwa hospitali kutokana na ugonjwa wa stroke

Zari alipoenda hospitalini kumwona Iva

Akiongea kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Diamond alieleza sababu zake za kukosa kupost chochote kumtakia hali Ivan Ssemwanga.

“Ni kweli mzazi wake Zari anaumwa, na yuko serious. Na kila siku huwa namuhimiza Zari akamuone mzazi mwenzie kwasababu najiuliza asingekuwa anaenda familia yangu ingemuonaje, kwa hiyo maskini dada wa watu kila siku huwa anaenda. Sijawahi mpigia simu kwasababu yuko serious sana na pia sikuweza kumpost kwasababu watu waneanza kusema labda natafuta kiki maskini ya Mungu kumbe wala,” Diamond alisema.

Diamond akiwa Clouds FM

 

Ray C ashindwa kuficha furaha yake baada ya Diamond kukiri hili

Rehema Chalamila maarufu kama Ray C ameishiwa na maneno ya kusema baada ya Diamond Platnumz kufunguka kuhusu nia yake kimuziki.

Diamond alisema nia yake ni kuinua wasanii wengi kumuziki kwani wao kama yeye wamelelewa kwa umaskini. Super star huyo alisema hayo akitangaza uzidunzi wa msanii mpya wa Wasafi.

“Panapo majaaliwa siku ya jumatatu kesho, ntakuwepo kwenye LEO TENA ya Clouds fm na familia nzima ya @Wcb_wasafi tukimtambulisha Kijana mwenzetu Mwingine Mpya toka Mtaani, ndani ya @Wcb_Wasafi….. Sisi ni vijana ambao tumekulia kwenye umaskini na bado tupo kwenye kupambana namna ya kujikwamua kwenye umasikini… na ndiomaana tunajitahidi kadri ya uwezo wetu kila tukiona kijana yoyote mwenye nia na kipaji kumsaidia kwa kadri ya uwezo wetu, ili nae aweze kutambulisha kazi zake, na Pengine Mwenyez Mungu akimjaalia nae awe mkombozi kwenye Familia yake….Sio jambo Rahisi ni gumu, lakini kwa Sapoti yenu naamini tunaweza lifanikisha…Siku zote naomba mkumbuke WCB_Wasafi sio ya Diamond, ni ya vijana wote wapambanaji…na ndiomaana kila siku nawaomba Muendelee kuniombea na Kunisapoti, kwani Sapoti yenu ndio itayo nifanya hata kesho niweze kukuchukua wewe ama ndugu yako ili aje kukitambulisha kipaji chake na Mwenyez Mungu akijaalia kufikia Malengo…… USIKOSE kusikiliza Leo tena ya @Cloudsfmtz saa nne Asubuhi…Shukran?” Diamond aliandika kwa Instagram.

Ray C alifurahiswa na maneno ya Diamond kwa kiasi kwamba akaamua kumsifu kwenye mitendao ya kijamii. Alisema roho ya Diamond hauna ubinafsi kabisa.

“Wakitokea wasanii wakubwa kama wewe na wakawa na moyo kama wako basi muziki wetu utafika mbali sana…Kaa na huyu kijana japo nusu Saa tu,utaelewa kwa nini nasema haya!!Kuna Ro!!!!Na kuna RoHo!!!Jamaa ana Roho ya Peke Yake Maskini!!!!Na Mengi Moyoni natamani niongee lakini Haya Yanatosha mdogo wangu!!Kumbuka Mwenye Hii Dunia alishasema ,Mtoaji hupewa Zaid na Zaid…… Mungu akutangulie katika kila ufanyalo Inshallah…” Alisema Ray C.

 

Picha ya msanii mpya wa WCB ambaye Diamond alimtambulisha leo

Jana Mai tarahe 21 Diamond alitangaza kuwa atamtambulisha msanii mpya kutoko lebo ya Wasafi akifanya mahojiano kwa Clouds FM.

“Panapo majaaliwa siku ya jumatatu kesho, ntakuwepo kwenye LEO TENA ya Clouds fm na familia nzima ya @Wcb_wasafi tukimtambulisha Kijana mwenzetu Mwingine Mpya toka Mtaani, ndani ya @Wcb_Wasafi….. Sisi ni vijana ambao tumekulia kwenye umaskini na bado tupo kwenye kupambana namna ya kujikwamua kwenye umasikini… na ndiomaana tunajitahidi kadri ya uwezo wetu kila tukiona kijana yoyote mwenye nia na kipaji kumsaidia kwa kadri ya uwezo wetu, ili nae aweze kutambulisha kazi zake, na Pengine Mwenyez Mungu akimjaalia nae awe mkombozi kwenye Familia yake….Sio jambo Rahisi ni gumu, lakini kwa Sapoti yenu naamini tunaweza lifanikisha…Siku zote naomba mkumbuke WCB_Wasafi sio ya Diamond, ni ya vijana wote wapambanaji…na ndiomaana kila siku nawaomba Muendelee kuniombea na Kunisapoti, kwani Sapoti yenu ndio itayo nifanya hata kesho niweze kukuchukua wewe ama ndugu yako ili aje kukitambulisha kipaji chake na Mwenyez Mungu akijaalia kufikia Malengo…… USIKOSE kusikiliza Leo tena ya @Cloudsfmtz saa nne Asubuhi…Shukran?” Diamond aliandika kwa Instagram.

Diamond akiwa Clouds FM leo Mai 22

Hit maker huyo wa ‘Marry You’ alienda kwa kituo cha Cloud FM akiwa na Rayvanny and Lava Lava – msanii mpya wa Wasafi.

Rayvanny and Diamond wakiwa Cloud FM

Lava Lava tayari ameachia wimbo wake mpya ‘Tuachane’ akiwa Clouds FM leo. Wimbo wake pia unapatikana kwenye tovuti la Wasafi.

Msanni mpya wa Wasafi Lava Lava

 

“Sasa aliokwambia namtaka Damond ni nani? Wema Sepetu awaonya mashabiki dhidi ya kumhusisha na Diamond Platnumz

Wema Sepetu amesisitiza kuwa uhusiano wake wa kimapenzi na Diamond Platnumz ulikamilika kabisa. Mwigizaji huyo wa filamu ya Bongo amesema anataka mume bora.

Wema na Diamond walikua wapenzi kabla ya mwimbaji huyo kumtema Wema na nafasi yake kuchukuliwa na Zari Hassan.

Mara nyingi watu husema kuwa Wema na Diamond bado wako na uhusiano wa kimapenzi ila wanachezea chini ya maji mapenzi yao isigunduliwe.

Diamond and Wema Sepetu

Wema amesisitiza kuwa yeye na Diamond hawana lolote tena, alisema hayo wakati akimjibu shabiki katika kurasa wake wa Instagram.

“Sasa baby aliokwambia namtaka Damond ni nani? Life has to go on, yule ni baba wa watoto wawili jamani. Its about time u guys accept that me and Naseeb no more. Mnachotakiwa kuniombea ni nipate mwanaume bora na siyo bora mwanaume na mwenye heshima zake,” aliandika Wema Sepetu Instagram.

Alichosema Rayvanny baada ya kuteuliwa kuwania tuzo la BET 2017

Diamond Platnumz amekosa kupata uteuzi kuwania tuzo la BET 2017 lakini Rayvanny ameteuliwa katika kitengo cha ‘Best International View’s Choices’ akiwa ni msanii pekee kutoka Afrika katika kitengo hicho.

Rayvanny aliambia Ayo TV alikuwa studio akirekodi ngoma mpya ndo habari ikamfikia kuwa ameteuliwa kuwania tuzo la BET.

Diamond ata hivyo hajateuliwa kuwania tuzo la BET 2017; hit maker huyo wa ‘Marry You’ amewahi kuteuliwa mara mbili (2014 na 2016) kuwania tuzo hilo kwa kitengo cha Best International Act: Africa.

Tazama orodha hio hapo chini uone wasanii kutoka Afrika ambao waliteuliwa kwa kitengo cha Best International Act: Africa 2017:

Best International Act: Africa

AKA (South Africa)

BABES WODUMO (South Africa)

DAVIDO (Nigeria)

NASTY C (South Africa)

STONEBWOY (Ghana)

TEKNO (Nigeria)

WIZKID (Nigeria)

MR EAZI (Nigeria)

 

Ray C, Wolper wachekeshwa na mavazi walizovaa Diamond, Wema Sepetu, Rayvanny kwenye party ya Mendez (Picha)

Meneja wa Diamond Sallam Sharaff maarufu kama Mendez alisherekea siku ya kuzaliwa kwake kwa kufanya party ambayo kila mtu alitakiwa kuvaa mavazi ya kizamani.

AY, Babu Tale, Rayvanny, Rich Mavoko, Wema Sepetu, Dogo Janja ni miongoni mwa watu waliohudhuria party hio ambayo ilifanyika katika Club Rouge usiku wa Mai tarehe kumi na moja.

Rayvanny
AY and Mendez
Diamond, AY na Babu Tale
Diamond
Ricardomomo na Babu Tale
Wema Sepetu
Rich Mavoko
Mendez
Dogo Janja, Diamond na Rayvanny
Babu Tale
Dogo Janja

 

Ray C na Wolper ni miongoni mwa watu waliochekeshwa na kufurahishwa na mavazi ya Diamond na watu wengine waliokuwepo kwa party ya Mendez.

wolperstylish: Ma nigga ma boss I love this boss of mine??hey ma nigga ur so speshoooooooooo? @diamondplatnumz ……

rayctanzania: ???????umewamaliza dogo langu!yani uwe unavaa hivyohivyo na viatu namna hiyo na nywele namna hiyo??

Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia aambia Bunge Diamond amekwepa kulipa kodi

Ni miezi mbili tu iliyopita ambapo Diamond alienda kwa makao makuu ya Mamlaka ya Mapato TRA baada ya kuitwa ili alelezee namna anavyopata mapato yake na namna gani analipa kodi ya serikali.

Diamond alipewa cheti na TRA kama dhibitisho kuwa analipa kodi ya serikali kama inavyohitajika na sheria ya Tanzania.

Diamond alipoitwa kwa makao makuu ya Mamlaka ya Mapato TRA

Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia hata hivyo jana aliambia Bunge kuwa Diamond anadaiwa na Mamlaka ya Mapato zaidi ya shilingi milioni 400.

Mheshimiwa Mtulia alidai kuwa hit maker huyo wa ‘Marry You’ alimwambia kwa sasa anadaiwa kodi ya zaidi ya shilingi milioni 400 na TRA.

Mbunge wa Kinondoni Maulid Mtulia

Mbunge huyo aliyasema hayo wakati wa mjadala wa bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ulipokuwa ukijadiliwa bungeni.

 

Shilole: Mimi namkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko Ali Kiba

Shilole ameeleza sababu ya kumkubali Diamond Platnumz kuliko Ali Kiba – wawili hao (Ali Kiba na Diamond) ni maadui wakubwa kimuziki.

Nani kati Diamond na Ali Kiba ndo mfalme wa muziki Tanzania? Mjadala huu huzua utata kila mara unapoulizwa. Mashabiki wa Diamond watasema Simba ndo anaweza na wale wa Ali Kiba watasema yeye ndo bingwa.

Zuwena Muhamed alimaarufu kama Shilole amesema yeye ni Team Diamond Platnumz. Akiongea kwenye kipindi cha Kikaangoni live kinachofanyika kupitia ukurasa wa facebook wa EATV, Shilole alisema yeye anamkubali sana Diamond.

“Mimi namkubali zaidi Diamond Platnumz kuliko Alikiba, nampenda Diamond kutoka na mambo yake na vile alivyo, kwa hiyo kila mtu ana watu anaowakubali na kuwapenda” alisema Shilole.

Alichosema Young Killer baada ya Diamond kuamua kutoa wimbo naye

Nyota ya Young Killer sasa inakaribia kung’aa vizuri, rapa huyo ataingia studio na Diamond Platnumz kurecord ngoma mpya itakayompa umaarufu nje ya Tanzania.

Msanii yeyote ambaye amewahi kufanya kazi na Diamond anajua vizuri thamani ya kumshirisha Simba kwa kolabo yoyote ile.

Young Killer

Young Killer sasa amefunguka kuhusu kazi atakayofanya na hit maker huyo wa ‘Marry You’. Rapa huyo alisema mama yake alifurahishwa sana na kitecho cha Diamond kuamua kumshirikisha kwenye moja kati ya nyimbo zake zinazokuja.

Akiongea na Bongo5 hapo jana Mai tarehe nne, Young Killer alimmwagia sifa Diamond na kumtaja kama msanii anayekuza vipaji Tanzania.

“Hiki kitendo kimenifanya nimuone Diamond Platnumz ni binadamu na ni mtu ambaye anastahili kuwepo sehemu ambayo yupo. Ni tukio ambalo limenitia faraja kiukweli hata mama yangu alivyosikia alifurahia sana na kumshukuru kwa kitendo ambacho amenifanyia,” alisema Young Killer.