Alikiba, Darassa, Diamond na Vanessa Wang’aa Kwa Tuzo Nchini Uganda

Wanamuziki wakali wa Bongo fleva kama Diamond, Ali kiba, Vanessa Mdee na Darassa wameng’aa kimataifa zaidi baada ya kila mmoja kujishindia tuzo za Hippo nchini Uganda.

Tuzo hizo zilifanyika usiku wa jana nchini Uganda ambapo baadhi ya wasanii waliopata Tuzo kutoka Tanzania ni kama vile Diamond, Ali Kiba, Vanessa Mdee na Darassa.

Vanessa Mdee ameibuka na tuzo ya heshima katika kipengele cha ‘East Africa Best Female Artist’ na Alikiba akiibuka na tuzo ya kipengele cha ‘Song of the Year Tanzania’ kupitia wimbo wake wa Seduce Me.

 

Diamond Platnumz ameshinda tuzo mbili mbili kwenye vipengele vya ‘Africa Song of The Year’ kupitia wimbo wake wa ‘Marry U’ aliomshirikisha Ne-Yo na ‘Best East Africa Video’ kupitia wimbo wa Eneka.

Darassa ameibuka kidedea kwenye kipengele cha ‘East African Super Hit’ na wimbo wake wa Muziki ambao amemshirikisha Ben Pol.

 

Saida Karoli atumia maneno kutoka kwa wimbo wa Darassa kwenye wimbo wake mpya

Saida Karoli amerejea katika ulingo wa muziki kwa kuachia wimbo mpya kali ambayo ni dhibitisho kuwa kipaji chake hakikupata kutu alipokua kimya.

Mkongwe huyo wa muziki wa asili ameachia wimbo mpya unaoitwa ‘Orugambo’  ambayo iliwekwa kwenye YouTube jana Jumatatu.

Karoli alitumia maneno kutoka kwa wimbo wa Darassa ‘Muziki’ kwenye wimbo wake mpya ‘Orugambo’ .

“Maisha na muziki, wacha maneno weka muziki x2” Saida Karoli aliimba kwa wimbo wake mpya.

Tazama wimbo hio kwenye video hapo chini: