Steve Nyerere:Tunaongoza kwa Kuonyesha Tamthilia Zenye Ubora.

Siku za nyuma kidogo Steve Nyerere alikuwa ni moja ya wasanii wa bongo movies ambao walikuwa wakilalamikia sana tasnia hiyo na kusema kuwa kwa muda mrefu tasnia hiyo imekuwa ikifanya kazi na wasanii wale wale na kurudia makosa makubwa kila siku kiasi kwamba watu wamechoka kuona wakifanya hayo  hivyo hiyo ni sababu kubwa ya kufakwa bongo movies.

Lakini siku za hapa karibuni msaniii huyo ambae ndio amekuwa kama baba katika bongo movies anasema kuwa kwa sasa kazi za tamthiliya zimekuwa zikifanya vizuri sana kiasi kwamba inawezekana kabisa kuwa Afrika Mashariki ikawa ndio inaongoza kwa tamthiliya nzuri na zenye ubora kuliko sehemu nyingine yoyote ile.

download latest music    

Steve Nyerere anasema kuwa kwa sasa wasanii wameanza kujirekebisha na kutaka kuinuka tasnia hiyo , hivyo wameanza kujituma na kujitutumuanili kufanya kazi itakayowalipa lakini pia kuwaweka mashabiki wao katika nafasi nzuri ya kuangalia tamthiliya.

Tumesimama sana kwa afrika mashariki na hata magharibi sisi ndio tunaongoza kwa kuonyesha tamthiliya zenye ubora ,inaonyesha ni kwa jinsi gani Tanzania kuna vipaji.

 

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.