Sitamani Kuona Mtoto Wangu Akiimba Muziki :-Nay wa Mitego
Msanii Nay wa mitego amefunguka na kusema kuwa hatamani kuona mtoto wake hata mmoja akijiingiza katika swala la muziki kwa sababu hataki yale aliyoyapitia yeye katika muziki yawapate watoto wake pia.
Nay anasema kuwa ingawa hatoweza kukataa kama mtoto wake yoyote atajiingiza katika muziki hivyo atamuunga mkono tu lakini hapendi iwe hivyo.
Natamani kuona siku moja wanangu wakipambana na maisha yao, wanakuwa na maisha na majina makubwa, ingawa ikitokea mmoja akijiingiza katika muziki ntamuunga mkono tu ingawa sitamani kuona hata mmoja wao akiijiingiza katika muziki.Na kwa sababu ya historia yangu sitamani mwanangu aje kuwa mwanamuziki.
Nay wa mitego ana watoto wawili wa kike na wa kiume.