“Sikuwahi kuwa mshabiki wa Diamond” Naibu Waziri wa Afya Hamis Kigwangalla atoa maoni yake kuhusu Chibu Perfume

Diamond alizindua manukato yake “Chibu Perfume” siku chache zilizopita. Staa huyo wa Bongofleva alifanya uzinduzi mkubwa, aliwaita wanahabari alipozindua Chibu Perfume.

Hatua hio ilifanya Diamond kutawala vichwa vya habari, Naibu Waziri wa Afya Hamis Kigwangalla ni miongoni mwa watu walitoa maoni yao kuhusu uzinduzi wa Chibu Perfume.

download latest music    

Bwana Kigwangalla alikiri hakuwa shabiki wa Diamond hapo mwanzoni lakini alianza kupenda muziki wake hivi karibuni.

Alimsifu Diamond kwa kuwa mwanamuziki timam na mwekezaji ambaye ni mfano mwema kwa vijana nchini Tanzania.

“Sikuwahi kuwa mshabiki wa msanii huyu kijana @diamondplatnumz, kama nilivyosema hapo nyuma kidogo, japokuwa nimekuwa nikifuatilia na ku-enjoy muziki wake; Ila toka nimeanza kumfuatilia nimegundua kuwa, this young man is not only a good entertainer, but also a talented entrepreneur and businessman. He does business in music, he does a business of entertainment. Sasa naona kupitia kipaji chake cha ujasiriamali, naona ameamua kuwa muwekezaji, an investor! This is incredible. Keep stepping up your game son, that’s the way to do it! Hakika wewe umetoka #NjeYaBox, na Mungu akuongoze ubaki huko huko juu, usishuke! I wish wasanii wenzako pia watoke nje ya box kifikra, wafanye biashara kwenye vipaji vyao, wageuze changamoto kuwa fursa, waache kulalamika, wapige kazi tu! #HapaKaziTu! Kwa sababu nyie watu mashuhuri mkigeuza crowds zenu kama chanzo cha solo la bidhaa zenu, kwa hakika mtafanikiwa sana! Changamoto kwenu wadogo zangu..” Hamis Kigwangalla alisema.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere