Shilole- Wivu Ndio Umempelekea Uchebe Kuwa Video King
Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa sababu za mume wake Asharaf Uchebe kuwa video king kwenye video yake.
Siku chache zilizopita Shilole ameachia wimbo wake mpya unaoenda kwa jina la ‘Champion’ na ndani ya video hiyo mumen wake Uchebe amesimama kama video king hali iliyopelekea mashabiki kuhisi huenda msanii huyo amejiingiza kwenye sanaa rasmi.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers , Shilole alisema kuwa, mumewe huyo huwa hapendi sana kumuona akishuti video na wanaume huku ‘akibambiwabambiwa’ hivyo ili kumfanya awe na amani ndipo akamtumia yeye kwenye video hiyo.
Ule wimbo kwanza nilimuimbia yeye, lakini Uchebe ana wivu sana, huwa hapendi kuona nashikwashikwa na wanaume kwenye video au hata kwenye steji, ndiyo maana nikaona kwa wimbo huu ambao nimemuimbia, siyo vibaya nikamtumia na kakinogesha kichupa ile mbaya”.