Shilole Afungukia Sababu Za Kutomzalia Uchebe
Msanii wa muziki wa Bongo fleva nchini Zuwena Mohamed maarufu Kama Shilole amefunguka na kuanika sababu zinazomfabya mpaka leo hii asimzalie mume Wake Ashraf Uchebe.
Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha Enews cha EATV, Shilole ameweka wazi kuwa sababu pekee iliyomfanya Mpaka sasa hajamzalia Mumewe Uchebe ni sababu anaamini Mungu bado hajambariki Mtoto kwa sasa kwani Mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu.
Lakini pia Shilole ameweka wazi kuwa wao Kama wana ndoa wamekuwa wakijaribu kwa kipindi kirefu sasa kutafuta Mtoto lakini majaaliwa ya Mwenyezi Mungu hayajatimia bado.
Sisi tulikuwa tunatafuta Tupate Mtoto lakini bado hatujajaliwa, unajua mtoto sio kwamba mtu unapachikwa tu, mtoto anatafutwa na hatafutwi siku moja watu wanakaa miaka hata 10 na hwapati Mtoto na wako kwenye ndoa, Mimi tayari Nina watoto wawili na hata hao wengine hawakupatikana hivi hivi”.
Shilole tayari ni mama wa watoto wawili wa kike aliozaa na aliyekuwa mume Wake ambaye pia alifariki Wiki chache zilizopita.