Shilole Afungukia Anachotamani Kufanya Kabla Ya Mwaka Kuisha

Msanii wa Muziki wa Bongo fleva na mjasiramali Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa anatamani sana mwaka huu usiishe kabla ya kuhamia Kwenye mjengo wake.

Mwezi uliopita Shilole aliweka wazi mjengo wake wa kifahari anaojenga kwa pesa anayopata Kupitia Muziki anaofanya na biashara zake kama kuuza chakula (Restaurant).

download latest music    

Kwenye moja ya Interview aliyofanya hivi Karibuni na gazeti la Dimba, Shilole, ambaye amekuwa akifanya vyema kupitia biashara yake ya chakula, amesema kikubwa anachofanya kwa sasa ni kuona ndani ya mwaka huu biashara hiyo inamwingizia pesa za kuweza kujenga nyumba yake.

Natamani sana nifikie kile nilichokusudia, nashukuru mpaka sasa naweza kusema biashara yangu inanilinda vya kutosha, nimefanya vingi kupitia chakula”.

Shilole amesisitiza kuwa lengo lake kuu ni kumaliza mwaka huu huku biashara zake zikiwa zimefanikiwa kwa asilimia 90 sambamba na kuhamia kwenye mjengo wake.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.