“Sarah Hajakasirika Nilivyokumbatiwa na Wolper”- Harmonize
Msanii wa muziki wa Bongo fleva kutokea katika label ya WCB Harmonize ameibuka na kudai kwamba Mpenzi Wake Sarah hajamind kitendo cha yeye kukumbatiana na Ex Wake Wolper.
Wikiend iliyopita mkoani Mtwara kwenye tamasha la Wasafi Festival Harmonize alirekodiwa akikumbatiana na Ex Wake Wolper wakati wa kusalimiana mara moja tetesi zilianza kusambaa kwamba wawili hao wamerudiana.
Tetesi hizo zilizimwa na Mpenzi wa Harmonize, Sarah ambaye Kupitia ukurasa wake wa Instagram alisema yeye na Harmonize hawajaachana na hawategemei kuachana na muda si mrefu angejiunga naye Mtwara kwa ajili ya shoo hiyo.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Harmonize alisisitiza yeye na Wolper ni washkaji tu na wapo kikazi ila Mpenzi Wake ni Sarah na hajamind alivyoona video za wawili hao kukumbatiana:
Wolper ni mtu wangu wa karibu na nilifurahi kumuona akishiriki tena na Wasafi na kuhusu Sarah najua hawezi kumaindi kwani anaelewa kuwa tupo Mtwara kikazi zaidi”.