Roma akamilisha Usajiri BASATA.
Msanii Roma Mkatoliki maefanikisha jukumu lake la kujisajili kama msanii rasmi wa tanzania katika tasnia ya muziki na kuwa kwa sasa anatambulika na BASATA na kazi zak zitakuwa zinzlindwa na baraza hilo.
Hayo yamekamilika siku ya march 5 mwaka huu baada ya kuagizwa kufanya hivyo na baraza siku chache zilizopita ambapo msanii huyo alikutana na uongozi wa BASATA na Naibu waziri wa habari kwa ajili ya kuzngumza mambo mbalimbali na pia kuongelea swala lake la kugfungiwa kwa muziki wake na yeye pia kufanya kazi za sanaa.
Roma ambae alikuwa amefungiwa kutokana na wimbo wake kukosa maadili na alipotakiwa kuurekebisha alichelewa kufanya hivyo lakini baadae alikuja na kutambua kosa lake hivyo kukaa chini na mamlaka husika hivyo kupata kibali cha kurudi kazini na kusamehewa adhabu yake.
Akiongea na waandishi wa habari katika usajiri huo, katibu mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza anasema kuwa “tunawaomba sana wasanii waje kufanya usajiri na pia kuleta nyimbo zake kukaguliwa mashairi ili kupelekwa kwa public na pia hata wa kazi za filamu ninawaomba sana kuna mamlaka husika “