Riyamma Asema ,Amelipwa Kunenepesha Mwili Wake.
Msanii wa bongo movies ambae anasifia kwa kuta vichambo vya hali ya juu katika filamu na sinema za kibongo Riyama Ally amefunguka na kusema kuwa kwa sasa watunwengi wamekuwa wakimsema vibaya kuhusu kunenepa kwake na kwamba anazidi kuwa mnene hivyo manyama uzembe yanazidi kuongezeka.
Riyamma amesema kuwa ni kweli kuwa kwa sasa amenenpa kwa sababu kuna kazi nyingi za filamu anafanya na katika scene mbalimbali anatakiwa acheze kama mama hivyo inamlazima kufanya hivyo kwa sababu hiyio ndio kazi yake na amelipwa kufanya hivyo.
Riyama anasema kuwa endapo atapunguza mwili wake basi hatoweza kuvaa uhusika wa kile kinachotakiwa kuigizwa katika tamthilia hizo ambazo amelipwa kufanya kazi.
Siwezi kupungua kwa sasa hata iweje,labda mpaka nipate kazi itakayo nifanya nicheze nikiwa nimepungua ndio nitapungua.lakini sasa hivi nimelipwa kuwa hivi nilivyo.-Alifunguka Riyama