Rammy Galis Alamba Shavu Nono
Muigizaji wa Bongo movie Rammy Galis amejikuta analamba Shavu nono baada ya kukabidhiwa ubalozi wa maduka ya City Mall na City Mall Cinema yaliyopo Mnazi mmoja jijini Dar Es Salaam.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Rammy amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa kupata nafasi hiyo kwani kwa upande wake inaweza kumtoa sehemu moja kwenda nyingine, jambo ambalo alikuwa akilitamani.
Ndoto yangu kubwa ilikuwa ni hiyo, lakini pia nafurahi filamu yangu niliyoigiza na marehemu Masogange (Agness Gerald) itaanza kuoneshwa kwenye ukumbi huo wa sinema wakati ninaizindua”.
Miezi michache baada ya Kifo Cha Agnes Masogange ambaye alikuwa mpenzi wake Rammy alitangaza kutoa Movie yao waliyofanya kwa pamoja kabla ya Kifo chake.