Najuta Kupoteza Miaka 6 Kwa Ajili ya Makomandoo-Muki

Baada ya habari kusambaa kuwa kundi la muziki  la Makomandoo limesambaratika  habari amabzo ziliwekwa wazi  na Fredy Whine ambae ni mmoja wa wasanii wanaounda kundi hilo, na  kusema kuwa kwa sasa kundi hilo limekufa kwa sababu mwenzake Muki yuko busy na familia na kwamba  familia yake inambana sana kufikia hatu akushindwa kufanya kazi.

Lakini baada ya taarifa hizo kusambaa , Muki pia ameamua kufunguka na kusema kuwa sio kweli kuwa familia imemfanya yeye na Fredy waachana na washindwe kufanya kazi za muziki.Hata hivyo Muki amesema kuwa alishangaa sana kuona habari kama hizo kwenye vyombo vya habari na hata ndugu zake walitaka kujua kama wamegombana.

download latest music    

 Alitaka kunipeleka polisi kisa gari,tukafanya nyimbo lakini nikawa nasikia anafuta sauti zangu,Nilimwambia kuwa nimeshachoka na isiwe shida itafika sehemu mimi nitaamua maamuzi magumu lakini kabla ya mimi kuamua nashukuru kaanza kuamua mwenzangu.

Ilo ni tatizo lingine ambalo ananitangazia kuhusu familia, kwamba inafanya  nisifanye muziki  lakini hata yeye ana familia pia na familia yake haijali kabisa, na ndio maana anaona mimi nimebanwa na familia , hakuna ukweli huo.

Baada ya kuongea hayo yote , Muki alisema kuwa sababu kubwa ya wao kugombana ni kwa sababu  msanii mwenzake huyo ana roho mbaya hivyo hawawezi kukaa wote na kufanya kazi.

Tatizo kubwa la ndugu yangu yule ana roho mbaya,mpaka mimi mwenyewe uwa namwambiaga kuwa wewe sidhani kama kwa roho yako hiyo tutaweza kufanikiwa kwa sababu mimi naona kabisa ambavyo mimi ninavyoshow love kwako.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.