Mzee Majuto Aomba Msaada wa Matibabu Nchini India
Msani wa maigizo nchini Mzee Majuto anaomba msaada wa kuomba kuchangiwa ela kwa ajili ya matibabu yake anayopaswa kufanyiwa nchini india haraka iwezekanavyo,Mzee Majuto ambae alikuwa akisumbuliwa na tezi duma na kisha kufanyiwa upasuaji January mwaka huu alikimbizwa tena hospitali hivi karibuni baada ya kuonekana kuwa hali yake inaaanza kubaidlika baada ya kidonda alichokwa amefanyiwa upasuaji kushindawa kufunga.
Baada ya kufanyiwa uchunguzi imebainika kuwa njia salama kabisa ya yeye kuendelea kutibiwa ni kwa kupoatawataalamu zaidi nchini india hivyo mzee majuto na familia yake wameomba msaada kwa watanzania ili kupata fedha kwa ajili ya shuguli hiyo.
Akiongea kwa kuthibitisha hilo, mtoto mkubwa wa Mzee Majuto amesma kuwa baba yake anahitaji fedha ili aweze kwenda nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.
Hata hivyo, kiongozi ambae amekuwa akiwakilisha wasanii wengine, steve nyerere anasema kuwa huu ndio wakati wa watu kujitokeza na kutoa misaada yao na sio kusubiri mpaka mtu apate matatizo makuwa zaidi au awe amekufa ndio watu waanze kujitokeza kwa kutoa misaada na kuposti katika mitandao kuonyesha masikitiko yao wakati alipokuwa hai walishindwa kumsaidia.