Muziki wa Bongo Fleva Mwisho ni 2018:Nay wa Mitego
Msanii Ney wa Mitego maefunguka na kusema kuwa muziki wa bongo fleva unakaribia kufa na wanaoufanya ufe ni watu wakubwa ambao hawataki kusahaurika.Ney wa mitego anasema kuwa muziki huu unapotezwa na watu wenye mamlaka makubwa serikalini.
Ney wa Mitego amesema kuwa muziki wa bongo fleva unaenda kupotea kama ambavyo inavyopotea sanaa ya bingo movie na wasanii wake wataanza kupotea pia.Hayo yote yamesemwa na Ney wa Mitego baada ya kuwepo kwa mjadala mkubwa wiki hii uliohusiha watangazaji wa Clouds radio na Baraza la Sanaa pamoja na Naibu Waziri wakizungumzia matatizo ya wasanii hasa sakata la kufungiwa kwa wasanii na nyimbo zao.
Katika mjadala huo watu wengi waliuliza ili kutaka kujua sheria na taratibu zinazotumiwa na baraza ili kufungia nyimbo na msanii na huku wakihoji kwanini BASATA wamekuwa wakisimamia kuhusu maadili tu na kuacha vitu vingine.
Hata hivyo majibu yaliyotolewa na Baraza pamoja na Naibu waziri hayakuonekana kuwaridhisha wasanii kwa sababu hata baada ya majadala huo bali kulikuwa na malalamiko juu ya maelezo yao.
Kwa mahojiano ya leo, mtakuwa mmeelewa tatizo ni nini, naona mwisho wa huu muziki wa bongo fleva utakwamia hapa 2018.mkubwa atabaki kuwa mkubwa tu na mdogo ataendelea kuwa mdogo , na tusivyo na umoja tutaendelea kuwa wadogo na tunakoelekea ni tunaenda kule walikoenda ndugu zetu bongo movies.