Mimba ya Agnes Bado Yamuumiza Kichwa Mbasha

Msanii wa nyimbo za injili, Mabasha  bado anaandamwa na skendo ya kutembea na mwanamitindo Agness na kumpa ujauzito ingawa kwa nyakati tofauti msanii huyo amekuwa akikanusha wao kuwa na mahusiano  nahata kumpa ujauzito mwanamitindo huyo.

Mbasha anasema kuwa yeye na agness hawajuani zaidi ya yeye kujua kuwa mwanamitindo huyo amekuwa kama shabiki yake na yeye amemjua kupitia mitandao ya kijamii tu.Mbasha amesema kuwa  tetesi zinazosambaa juu yake hazina ukweli wowte na hawajawahi kuwa na ukaribu huo.

download latest music    

Agness namjua kama shabiki yangu kupitia kitandao ya kijamii tu,sasa sijui mambo yamegeuka vipi mpaka kufikia hatua ya kuambiwa kuwa mimi nina mahusiano nae.sijawahi kuwa na mahusiano na agnes wala kuwa na kitu chochote kinachoashiria mapenzi.

Sitegemei kupata nae mtoto kama watu wanavyosema kwa sababu sijawahi kuwa na mahusiano na mwanadada huyo,sina mahusiano nae huyo dada ni shabiki yangu tu.-Alisema Mbasha alipokuwa anaongea na Enews ya EATV.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.