Maya Akanusha Kumchamba JB
Mwana maigizo Mayasa Mrisho amefunguka na kujibu tuhuma za mashabiki kuhusu kumchamba msanii mwenzake jacb steven hivi karibuni na kusema kuwa waliotasfiri vibaya maneno yake walikosea kwa sababu sivyo alivyomaanisha.
katika ukurasa wake wa instagram maya aliweka picha ya Jb na kuandika”wewe baba wewe sisi tumekukosea nini wewe wa kutufanyia vile sisi, au unataka tukuanike humu walimwengu wajue, hayaturudishe kabla ya saa mbili , otherwise”
Hata baada ya kuulizwa , Mayasa alisema kuwa maneno hayo yalikuwa ni ya utani kwa kuwa jb ni kama baba yao na wameshazoea kumtania.
unajua kuwa jb ni kama baba yetu sisi wote na tulishazoea kumtania kila siku kwahiyo ile ilikuwa ni utani tu,hivyo mashabiki wangu wasidhani kama vile nilikuwa ninamaanisha kitu cha maana sana.