Malaika Afungukia Ukimya Wake
Msanii wa muziki wa Bongo fleva aliyewahi kutamba na kibao chake cha ‘Rarua rarua’ Malaika amefunguka na kuweka wazi sababu iliyomfanya mpaka akapotea kwenye gemu.
Malaika amesema kuwa ameamua kukaa kimya kwa muda mrefu ili kuangalia upepo wa gemu unaendaje kwani gemu inabadilika kila siku.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Malaika Malaika alisema kuwa anajua mashabiki wake wanajiuliza kwa nini hasikiki tena kwenye muziki lakini ukweli ni kwamba yupo anaangalia njia nzuri ya kuwafurahisha mashabiki wake.
Japokuwa nasafiri huku na kule lakini yote hiyo ni kuangalia upepo wa muziki unavyokwenda na ni kitu gani mashabiki wanakitaka kwa hivi sasa kama ni Singeli, Mduara au miondoko mingine yoyote ili niweze kutoka tofauti”.