Madam Florah Amjibu Emmanuel Mbasha Kuhusu Kumnyima Mtoto.
msanii wa nyimbo za injili nchini , Madam Florah ambae hapo awli alikuwa akijulikanakama Florah Mbasha ameamua kumjibu mzazi mwenzie , ambae pia alikuwa mme wake wa ndoa Emmnanuel Mbasha kuhusu lawama zake alikuwa amemtupia katika mtandao wa instagram siku ya wanawake duniani kuhusu kumnyima kumuona mtoto.
Madam Florah amesema kuwa hawezi kuzungumzia maswala nyeti kama hayo katika mitandao ya kijamii, wala katika vyombo vya habari juu ya swala hilo kwa sababu hata kama Emmanuel aliruhusiwa kumuona mtoto na mahakama lakini hakuruhusiwa na mahakama hiyo instahram kwaio hawezi kuyasema hayo huko.
siwezi kuzungumzia hilo swala katika vyombo vya habari hata siku moja,hilo swala ameliongelea instagram na mimi ningelitolea instagram, na ukweli hamuujui ila siis ndio tunaujua ukweli.na kama mahakama iliamua hivyo na yeye kaamua kuandika instagram basi sawa acha aandiki ila siwezi kuliweka wazi.
Emmanuel Mbasha na Flora walibahatika kupta mtoto moja kipindi cha ndoa yao , lakini walipokuwa wanapeana talaka mahakama iliamuru mtoto akae na mama yake kutokana na umri wa mtoto na baada ya hapo Madam Florah aliamua kuolewa na mwanaume mwingine.
Hivi siku za karibuni emmanuel alifunga katika mitandao ya kijamii na kusema kuwa mama wa mtoto huyo amekuwa akiakaidi agizo la mahakama la kumruhusu yeye kumuona mtoto na kusema kwa hana njia nyingine yoyote ya kumtumia ujumbe Florah zaidi ya hiyo ya instagram.