Jacqueline Wolper Ahaidi Kupambana na Marafiki Wanafki
Msanii wa filamu za Bongo Movie na mwanamitindo maarufu Jacqueline Wolper ametoa neno kwa marafiki wote ambao wamekuwa na tabia za kinafki na kuhaidi kupambana nao.
Wolper amefunguka na kudai siku akimkamata mtu ambaye wanafahamiana vizuri akiwa anamsema kwenye Mtandao wa Instagram atafurahia shoo kwa atakachomfanya.
Kwenye mahojiano yake na Global Publishers, Wolper kama mtu mnajuana na ukaona amekosea ni vyema ukamfuata mwenyewe na kumwambia kuliko kuandika unavyotaka Instagram kwani huo ni unafiki.
Siamini kabisa mtu mwenye mapenzi ya dhati na wewe anaweza kukuandikia ujumbe kwenye Instagram. Mimi huo ninauita unafiki na siku nikimkamata mtu wa aina hiyo atanijua“.
Siku chache zilizopita Wolper aliingia kwenye mgogoro na msanii mwenzake Esha Buheti baada ya kuamua kumsema Wema Kupitia Kwenye ukurasa wake wa Instagram jambo ambalo Wolper alidai hajapenda na kumtaka Esha amfuate pembeni na kumsema Wema badala ya kumsema Instagram.