Izzo Business- Siamini Katika Nguvu Ya Kiki Kwenye Sanaa
Msanii wa muziki wa hop hop nchini Izzo Business amefunguka kuhusu ukimya wake kwenye gems anapokuwa Hana nyimbo inayofanya vizuri kwenye vyombo vya habari lakini pia suala la Kiki.
Wasanii wengi wamekuwa wakitafuta kiki am app wamekuwa wakitengeneza skendo mbali mbali ambazo zinakuwa nje ya Sanaa ilimradi tu waendelee kuongelewa hasa kwenye mitandao ya kijamii.
Katika mahojiano yake na Gazeti la Risasi Vibes, Izzo Business alifunguka Baada ya kuulizwa sababu za kupotea kabisa anapokuwa hana nyimbo inayohit kwenye media:
Unajua kila mtu ana life style yake ambayo yeye anapenda kuishi na mara nyingi huwa mimi sipendi kuishi uongo, mimi napenda kuishi maisha yangu ambayo nayamudu siyo ya kujioneshaonesha kama sina kitu cha umuhimu au ulazima wa kufanya hivyo“.
Lakini pia Izzo alifunguka na kuweka wazi kuwa yeye sio mtu wa kutafuta Kiki na haamini sana kwenye Kiki Kiki za Sanaa:
Siamini sana kwenye kiki kwa sababu siku zote kazi nzuri inajiuza tu hata bila kiki. Unajua kiki ni ‘fifty fifty’ inaweza ikakupandisha unapotaka au ikakushusha tofauti na pale ambapo ulikuwepo na kila mtu ana mazingira na staili ambayo alianza sanaa yake kwa hiyo mimi kiki hapana kwakweli, kazi kama nzuri watu watasapoti tu ikiwa haijafikia kiwango, basi tutarudi studio kufanya kazi mpya“.