Hawa Atoa Shukrani Zake Kwa Diamond na WCB Baada Ya Kumaliza Matibabu
Msanii wa Bongo fleva Hawa Said maarufu kama Hawa ntarejea wa Diamond amevunja ukimya Mara Baada ya kumaliza matibabu nchini India na kumshukuru Diamond na WCB.
Msanii Diamond Platnumz na timu nzima ya WCB ndio ilisimamia matibabu yote ya Hawa mpaka anapiga kabisa Baada ya kuugua mpaka kutaka kufa miezi michache iliyopita.
Mrembo huyo amemshukuru Mungu pamoja na Watanzania kwa dua zao kwani mpaka sasa anaendelea vizuri na uvimbe wa tumbo umeondoka kwa asilimia kubwa.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Babu Tale ameweka wazi salamu kutoka kwa Hawa:
https://www.instagram.com/p/BqM4FSDlEiw/?utm_source=ig_share_sheet&igshid=1ex61xjcr1qbp
Awali msanii huyo wa kike aliripotiwa kuumwa ugonjwa wa ini lakini alipofanyiwa vipimo nchini India walimkuta na ugonjwa wa moyo.