Mobetto Apata VISA Ya Marekani Baada Ya Zari na Wema Kupigwa Chini

Mwanamitindo na Msanii wa Bongo fleva  Hamisa Mobetto amewabwaga mahasimu wake wakubwa Zari The Bosslady na Wema Sepetu na Kufanikiwa kupata visa ya kwenda Marekani.

Hamisa amewaacha mbali Zari na Wema baada ya kujipatia VISA yake ya kuingia nchini Marekani kwa ajili ya kupiga kazi.

download latest music    

Miezi michache iliyopita Wema Sepetu alitangaza kuwa atakuwa nchini Marekani kwa ajili ya kufanya appearance Kwenye Tanzania day lakini hilo halikufanikiwa baada ya kunyimwa VISA ya kwenda nchini humo.

Lakini vivyo hivyo ilikuwa kwa Zari ambaye Miezi michache nyuma alitangaza kuwapeleka Tiffah na Nillan kwa Diamond aliyekuwa nchini Marekani Kwenye ‘A Boy from Tandale Tour’ lakini baadae ilishindikana baada ya Zari kunyimwa VISA ya kuingia nchini Marekani.

Hamisa ameonekana kuwashinda mahasimu wake hao kwani hivi sasa yupo njiani kuelekea nchini Marekani kwa ajili ya appearance katika miji mbali mbali.

 

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.