Diamond Platnumz Atoa Kilio Chake Kwa Raisi Jakaya Kikwete
Msanii wa Muziki wa Bongo fleva Naseeb Abdul maarufu kama Diamond Platnumz ameandika waraka mzito kuhusu muziki wa Bongo fleva na mchango wa Rais Jakaya Kikwete.
Raisi mstaafu Jakaya Kikwete ambaye alikuwa mdau mkubwa sana wa Muziki wa Bongo fleva alikuwa anashehwrekea siku yake ya kuzaliwa jana na wasanii mbali mbali walimkumbuka akiwemo Diamond.
Diamond Kupitia ukurasa wake wa Instagram alikumbuka mchango mkubwa wa Raisi Kikwete kwa muziki wa Bongo fleva ambapo ameikosoa serikali ya sasa kwa kutofanya hivyo.
Miezi michache iliyopita serikali ilitangaza kuacha kuwatumia wasanii wa filamu na muziki na Bongo fleva katika kampeni zao za kisiasa hasa katika chaguzi kuu hii ni baada ya skendo zilizotokea baada ya kampeni za mwaka 2015.