Chuchu Hansy Adai Yeye na Ray Tayari ni Kama Mume na Mke

Muigizaji wa Bongo movie Chuchu Hansy ameibuka na kudai kuwa yeye na mzazi mwenzake staa wa Bongo movie Vicent Kigosi ‘Ray’ kisheria tayari ni mume na Mke bado tu kufanya sherehe.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake na gazeti Amani, Chuchu alisema kuwa japokuwa wao na Ray wamezaa lakini wamekuwa ni kama marafiki sana na watu wanaoelewana hivyo imebaki tu sherehe.

Unajua mimi na Ray hatujaamua kuweka wazi tu au tufanye sherehe kwa sababu tumekaa pamoja muda mrefu sana yaani kisheria ni mke na mume hapa kwa mujibu wa sheria, siwezi kusema sherehe ni lini lakini wasubiri”.

Ray na Chuchu wamekuwa Kwenye Mahusiano kwa miaka mingi na kufanikiwa kuzaa mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Jaden.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.