Bill Nas Aanika Majibu Yake Ya Ukimwi
Msanii wa muziki Bongo fleva William Nicholaus maarufu kwa Jina la usanii kama Bill Nas ameanika hadharani majibu yake ya virusi vya Ukimwi mara baada ya kupima.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Bill Nas avowals taarifa mashabiki zake kwa uwamuzi wake wa kwenda kupima afya yake na baada ya kupata matokeo yake aliyaanika pia.
Bill nas amewaasa mashabiki zake kwenda kupima ugonjwa huo na kuwaambia kuwa kila mmoja ni muhimu kujua hali ya afya yake.
Bill Nas ameungana na Listi ya wasanii wengi ambao siku za hivi karibuni wameonekana wakiwa wanapima Ukimwi na kisha kuyaachia majibu yao hadharani.