Aliyekuwa meneja wa Harmonize Ayakwaa Maneno ya Mashabiki.
Aliyewahi kuwa meneja ya msanii Harmonize amejikuta akiingia katika wakati mgumu hasa baada ya meneja huyo kusema kuwa sababu kubwa iliyomfanya aachane na msanii Harmonzie na kuacha kumuongoza ni kutokana na taba ya msanii huyo kubadilika kutokana na pesa.
Meneja huyo anasema kuwa sababu kubwa ni kuangalia tangu ameanza kufanya kazi na kijana huyo hakuwa kama alivyo sasa hivi kwa sababu hapo awali alikuwa akijituma na kufanya kazi hata kusikilizana lakini kadri siku zinavyozidi kwenda na mafanikio kuongezeka ndivyo anavyozidi kushusha nidhamu ya kazi.
Naelewa kuwa ni kijana mdogo ambae ametoka katika familia ya kimasiki lakini , utajiri , umaarufu na mafanikio aliyyapata yamemfanya na kumuathiri tabia yake.
Maneno hayo yamewafanya mashabiki kumshambulia meneja huyo huku wakisema sababu kubwa ni yeye na wala sio msanii wao.