Waliotaka Kumshusha Aslay Wamekwama Kwa Hili

Msanii wa Bongo Fleva anaefanya vizuri sana katika muziki kwa sasa na amekuwa akipendwa na mashabiki kutokana na uzuri wa nyimbo zake, Aslay ambae hivi karibuni amekuwa akitoa nyimbo mfululizo na kupokelewa vizuri kabisa na mashabiki  bila kujali interval ya wimbo mmoja na mwingine.

Siku chache zilizopita baada ya Aslay kutoa wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la Natamba, na kuanza kufanya vizuri katika channel ya Youtube, iliripotiwa kuwa wimbo huo umefungiwa katika channel iyo kuwa hauruhusiwi kuonekana public kwa watu bali watazamaji lazima wawe juu ya miaka 18, kwa sheria za channel iyo iliwataka waangaliaji kujisalili na kufuata masharti ndipo waweze kuona au kuupakua kutoka katika account hiyo.

download latest music    

Hata hivyo, baada ya kufuatilia kwa muda na baadhi ya watu wake wa karibu kuangaika, wakishirikiana na bosi wake anaejulikana kama MxCarterm alitatua tatizo hilo na kuwajulisha mashabiki wake katika ukurasa wake wa instagaram.

Akiandika katika ukurasa wake wa instagram baada ya kutatua tatizo ilo, MxCarter aliandika”usiyempenda karudi” huku akiweka picha ya msanii huyo.

Akaunti hiyo ya msanii Aslay inaonekana kuwa hacked na watu wasiojulikana huku lengo lao likiwa halijajulikana , lakini kitendo kama icho kinafanya kutokuonekana kwa musiki huo kwa mashabiki hivyo kushusha idadi ya mashabiki,Aslay kwa sasa amekuwa akifanya vizuri sana katika kazi zake pamoja na kuvunjika kwa kundi lao la Ya Moto Band ambalo lilikuwa pia lilikuwa likifanya vizuri, lakini hata baada ya kuvunjika kwa kundi hilo , Aslay amekuwa akikaririwa akisema haijamfanya hashindwe kuendelza muziki wake.

Hivyo kama kuna watu walikuwa na lengo la kufanya muziki wa Aslay kushindwa kuwafikia mashabiki , basi swala hilo halijafanikiwa.Pia tunatoa pole kwa msanii huyo kwa maswahibu hayo yaliyomkuta.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.