Nedy music Atamani Mtoto
Baada ya kushinda Tuzo Kutoka nchini Ghana msanii Nedy Music sasa ametangaza kilio chake kuwa mwaka huu anahitaji kupata mtoto ingawa wa kuzaa nae hajamjua.
Akiwa kwenye mahojiano Nedy Music maarufu kwa sasa kama mpemba mmoja amesema “Natamani kupata mtoto mwaka huu na kabla ya mwezi wa 12 ila bado sijapata mama wa huyo mtoto natamani nimpate kipindi hichi”
Aidha Nedy amekuwa mtu ambaye hapendi kuweka mahusiano yake hadharani japo huko nyuma alishakuwa na tetesi za kutoka na binti mmoja mwenye pesa zake ni mtazania ambaye anaishi Dubai.