Sasha Akiri Kununuliwa Gari na Kigogo Mkubwa Serikalini
Video Vixen anayesumbua kwa umbo lake matata Sasha Kassim ameibuka na kudai Hivi sasa anamiliki gari la kifahari alilozawadiwa na Waziri katika siku yake ya kuzaliwa januari 1.
Kwenye mahojiano aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Sasha alisema kuwa anamshukuru Mungu mwaka ameuanza vizuri kwani amepewa gari aina ya Toyota Harrier (New Model) na mwanaume huyo ambaye pia amemuahidi kumuoa.
Unajua huyu ni waziri mimi naona sio vema kumuanika kwa jina ila kwa sababu ana nia ya kunioa, mtamuona hivi karibuni kwani mambo ya kuficha ficha hayatahitajika tena”.
Gazeti la Ijumaa linaripoti kuwa Sasha ameshawahi kutangaza kuwa ndani ya miaka miwili ameshahaidiwa kuolewa na wanaume watatu tofauti wakiwemo wanaume wa nje ya nchi lakini mpaka leo hii hakuna hata aliyemvisha pete ya uchumba zaidi ya kumdanganya na kuingia mitini.
Lakini pia Sasha alipotakiwa kumuonesha mwanaume huyo kwa picha aliingia mitini na kudai kuwa kwa sababu ni waziri hawezi kumuanika kwa sasa.