Fella Hamiliki Muziki,-Chambuso Aongea.
Ya Moto Band ni moja ya kundi kubwa la muziki lililokuwa limeteka sana hisia za mashabiki wa Bongo Fleva nchini kutokanana kazi nzuri waliyokuwa wakiifanya katika muziki , kundi hilo ambalo liliundwa na vijana wadogo waliokuwa wanachipukia kimuziki lakini walikuwa wakifanya vizuri. kKwa bahati mbaya kundi ilo lilikuja kusambaratika na vijana wote kuanza kufanya kazi kwa kujitegemea huku Aslay akiwa chini ya menejenti mpya ya Chambuso.
Kabla ya kundi ilo kuvunjika lilikuwa likiongozwa na Chambuso pamoja na Mkubwa Fela na kuunda lebel iliyokuwa ikijulikana kama Mkubwa na wanawe na moja kati ya kundi lililoundwa lilikuwa ni Ya Moto Band, ambalo hivi sasa limekufa.Hata hivyo baada ya kundi kuvunjika Chambuso aliamua kuanzisha lebel yake mpya na alipomchukia Aslay kama msanii wake.
Kumekuwa na tetesi zinazoendelea kwa baaadhi ya watu wakisema kwa endapo msanii akitoka kwa Mkubwa Fellla basi na muziki wake umekufa, Chambuso anakanusa maneno hayo na kusema kuwa“Wanaosema kwamba muziki upo kwa peke yake, kwamba ukianzia kwake na ukatoka basi hautaweza kufanya vizuri tena, wanakosea na hakuna kitu kama hicho”
Chambuso anasema kuwa mfano mkubwa ni kutoka kwa aslay ambae ametoka kwa mkubwa fella na sasa hivi anafanua vizuri na kazi zake za kimuziki “Mbona Aslay anafanya vizuri sana na hayupo kwa Fella? Msisahau kwamba hata yeye huu muziki alizaliwa na akaukuta, kivipi ishindikane msanii kutoboa kisa hafanyi kazi naye, hicho kitu sikiamini.”anaongezea Chambuso
Hata hivyo maneno ya meneja mpya wa Aslay yanaweza kuthibitika kwa sababu tangu aslay amekuwa na menejiment mpya amekuwa akifanya vizuri na kila siku amekuwa akitoa nyimbo mpya ambazo zinapendwa sana na mashabiki, hivyo kufanikiwa kimuziki kwa msanii itategemea na nidhamu na juhudi anazokuwa nazo msanii binafsi katika kuifanya kazi yake ya sanaa.Tangu kuvunjika kwa kundi ilo Aslay ndio anayesikika sana katika muziki akifatiwa na Beka ambae pia ametoa wimbo mpya wa Libebe na Sikinai hivi karibuni.