Diamond Amtupia Dongo Hamisa Baada Ya Kumuanika Mpenzi Wake
Msanii wa muziki wa Bongo fleva Diamond Platnumz amemtupia dongo zito aliyekuwa Mpenzi Wake na mzazi mwenzake Hamisa Mobetto Baada ya kumuanika mpenzi wake.
Wiki iliyopita Hamisa alimtambulisha rasmi Mpenzi Wake mpya anajulikana Kama Josh Adeyeye ambaye amekutana naye nchini Marekani alikoenda kwa ajili ya kupiga shoo.
Diamond ameibuka na kumtupia dongo zito Hamisa Baada ya Stori za Hamisa na Josh kupamba moto kola kona kwenye mitandao ya kijamii.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diamond ameandika:
Najua mwili wangu ni mtamu, na najua bado unanitamani, ila usije ukadanganyika, hauwezi kuhimili stress“.
Hamisa na Diamond waliachana miezi michache iliyopita Baada ya kukiri kuwa kwenye mahusiano kwa miaka kumi ambapo Hamisa alikiri kumuacha Diamond Baada ya kuona hana muelekeo naye.