Aliyefungia Wasanii Na Nyimbo Zao sio Mh .Shonza.

Naibu waziri wa habari na michezo Mh Juliana Shonza amefunguka  na kusema kuwa aliyefungia nyimbo za wasanii na baadhi ya wasanii kufanya kazi sio yeye kama watu wanavyofikiria ila ni mamalaka inayohusika na swala hilo.

Juliana Shonza ameamua kufunguka hayo siku chache baada ya msanii Diamond Platinumz kwenda katika media na mitandao ya kijamii kulalamika kuhusu kufungiwa kwa nyimbo zake na kufungiwa kwa mwenzo Roma Mkatoliki.

download latest music    

Amewataka wasanii na wananchi kwa ujumla kujua kuwa sio yeye aliyefanya hivyo bali ni mamlaka husika.”Aliyewafungia wasanii sio shonza bali ni mamlaka husika na kama mnavyoona sasa hivi hadi mamlaka ya mawasiliano tanzania , TCRA imeingilia kati swala hilo.sasa  mtu anarusa tuhuma kunilaumu  anakuwa hanitendei haki kwa kweli”.

Kumekuwa na malalamiko mengi sana kutoka kwa wasanii wakielekeza  tuhuma zao kwa naibu waziri Juliana Shonza juu ya kufungiwa kwa wasanii wengi wa muziki kutokana na swala la maadili.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.