Lebel ya Young Dee Yalia na BASATA
Uongozi wa msanii Young dee umefunguka kwa mara ya kwanza baada ya kufungiwa kwa wimbo wa msanii wa Young dee unaojuliknakama bongo bahati mbaya ambao unasemekanakuwa hauna uzalendo, kwa muda wa usiojulikana kupigwa katika vituo mbalimbali vya habari au kusikika ukipigwa sehemu yoyote.
uongozi wa msnaii huyo umeandika barua ya wazi kwa BASATA NA kusema ;-
Kama mwekezaji kupitia tasnia ya muziki napenda kufikisha kilio changu kweny BASATA,kwa sababu pale ambapo muziki wa king cash unapofungiwa ina maana pia biashara ya king cash imefungiwa pia.hii inamaanisha nini/ hii inamaanisha kuwa kama itafungiwa muziki 100 basi familia zaidi zitakuwa zimeathirika na mnyororo huo.
ukiangalia upande wa biashara, king cash ni kampuni inayoongeza pia ajira kwa kuaajiri watu wengi na kujiajiri ili kutekeleza sera ya hapa kazi tu.badala yake mnaona ni kama kitu cha kawaida tu cha kukosoa na kufungia bila kuangalia ni ubunifu wa aiana gani ulitumika kufanya utunzi wa nyimbi hizo, tena mnafungia kwa kigezo cha kuwa wimbo hauendani na uzalendo, kwlei jamani tutafika namna hii.
kama hamjui kuwa kila wimbo unabajeti yake katika uzalishaji na kuitangaza na matarajio ya kipato kitakacho zalishwa na wimbo hiyo ambayo faida u=itatumika kuendesha maisha ya msanii na kutengeneza sasa mnapofungia nyimbo mnataka tuache kazi ya muziki na familia zetu zitaishije.kingine ebu tujifunze kupitia nchi jirani kwanza , tunaweza kuwa na busara katika hili na ushirikiano ni jambo katika kukuza ustawi wa sanaa yetu.
Asante Sana
KingCcash
Dar Es Salaam