Irene Atoa Sababu ya Mama Yake Kutohudhuria Harusi Yake.

Kama ambavyo watu wengi hawakutaka kuamini kuhusu kufunga ndoa kwa Irene Uwoya na Dogo Janja , pia yalizuka maneno kuwa mama wa urene uwoya hakuhudhuria katika harusi hiyo kwa  sababu hakupenda mwanae kufunga ndoa na Dogo Janja kwa kuwa yeye hakuwahi kuwatenganisha mwanae na Ndikumana ambae alifunga ndoa ya Irene Uwoya kanisani.

Hata hivyo Irene Uwoya amezima maneno hayo baada ya kufunguka sababu iliyomfanya mama yake kutohudhuria katika harusi yao na kusema kuwa mama yake amekuwa ni mtu wa kusafiri kila siku hivyo hakuwepo jijini ndio maana hakuweza kutokea katika harusi yao.

download latest music    

Hakuwepo kwaio hakuweza kushiriki kwa sababu mama yangu ni mtu wa kusafiri safiri kila siku,kwaio hakuwepo tanzania lakini ndoa yangu aliibariki kabisa.mama anenda anarudi na kazi zinakuwa nyingi kwaio hatujapa nafasi ya kutulia na kusema kuwa twende lakini ni mara nyingi mimi na yeye tunaendaga nyumba na baba anauwepo hata kama mama hayupo.-Aliongea Irene Uwoya walipokuwa na mahojiano katika kipindi cha leo tena cha Clouds Radio

Lakini pia Irene alisema kuwa marehemu mzazi mwenzie alikuwa akisema maneno mengi sana katika mitandao ya kijamii kuhusu yeye na kumnyima mtoto lakini ukweli ni kwamba alikuwa akimuona mtoto na hata mara nyingin alikuwa akitumia gari yake anapokuwa Tanzania.

 

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.