BET Waonyesha Kumtambua Diamond na Kazi Zake.
Diamond wiki yote iliyopita ameonekana kuwa na trending kubwa katika mitandao ya kijamii hasa baada ya kufanya uzinduzi wa album yake mpya huku nchini kenya na kuzoa mashabiki kibao huku watu mbalimbali wakizidi kumuongelea katika vyombo vya habari na katika mitandao ya kijamii.
Kituo kikubwa cha habari nchi cha BET nacho hakikuwa nyuma kuonyesha kufurahishwa na kazi za msanii Diamond kwa kumpongeza hasa baada ya nyimbo zake tano kuonekana katika list ya nyimbo bora za itune katika nchi ya Burkina Faso.
katika ukurasa wao wa twitter , BET waliandika congratulations @diamondplatinumz for having first 5 songs on the Burkina Faso iTunes top song list #winning.
Wiki hii pia Diamond aliachia wimbo wake mpya wa african beauty ambao amemshirikisha Omarion ambae pia alikuwepo katika uzinduzi wa album yake huko nchini Kenya na kufanya Diamond kuendelea kuwa na trending katika mitandao.